Matthew 18:1-5
Aliye Mkuu Katika Ufalme Wa Mbinguni
(Marko 9:33-37; Luka 9:46-48)
1 aWakati huo, wanafunzi wakamjia Isa na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?” 2Isa akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao. 3 bNaye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni. 4 cKwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni. 5 d“Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
Copyright information for
SwhKC